Washiriki katika Kulisha Akili, Kupambana na NjaaMradi wa Kulisha Akili, Kupambana na Njaa ulianzishwa na kundi la vyama vya kimataifa visivyo vya kiserikali ambavyo vimeungana pamoja ili kusaidia kumaliza njaa na ukosefu wa lishe bora kupitia elimu. Washiriki wanaamini katika kuja pamoja katika ushirikiano wa nguvu na ujuzi na dunia isiyo na njaa inaweza kupatikana kwa haraka na kwa mafanikio badala ya kila shirika kufanya kazi pekee yake. Shirikisho la Waalimu wa KimarekaniShirikisho la Kimarekani la Waalimu ni Chama Cha wafanyikazi kinachowakilisha zaidi ya wanachama Milioni moja katika nyanja za elimu K-12 (Waalimu na walio kama wataalam) Serikali za nchi, elimu ya juu na vyama vya wauguzi na taaluma za utabibu. Shirikisho la AFR lilianzishwa mnano mwaka wa 1916 na linajulikana kwa maadili ya kidemokrasi na kazi nzuri kwa niaba ya wanachama wake, na athari kubwa kwa viwango na mienendo ya kitaalamu katika mahali pa kazi wanachama. 555 New Jersey Avenue, NW, Washington, DC
20001-2079 (USA) Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO)FAO ilianzishwa mnamo mwaka wa 1945 na lengo la kuinua viwango vya lishe bora na maisha, kuongeza uzalishaji wa kilimo na kuboresha hali ya maisha ya wakazi wa mashambani. FAO ina wafanyikazi kote duniani na ina wananchi wanachama 180. Jumuiya ya Ulaya na FAO hulenga kupunguza ufukara na njaa kwa kuendeleza maendeleo ya kilimo, lishe bora na kutafuta kuwepo chakula cha kutosha – chakula kipatikane kwa watu wote wanapokihitaji kwa maisha bora.
Viale delle Terme di Caracalla, 00100 Rome (Italie)
Mavuno ya wakati ujaoMavuno ya wakati ujao hulenga kujenga dunia yenye kiasi cha chini cha umaskini, familia ya binadamu yenye afya bora watoto wenye afya nzuri na mazingira bora kwa kuongeza kiwango cha uelewa na kuunga mkono juhudi za utafiti wa kisayansi. Husaidia kuleta matokeo ya utafiti kwa jamii za mashambani katika nchi zinazoendelea na pia kufanya juhudi kusomesha watoto na watu wazima kuhusu umuhimu wa kilisha dunia na kulinda ulimwengu. PMB 238 2020 Pennsylvania Ave NW Washington, DC,
20006-1846, USA Chuo cha Kimataifa cha Sera ya Chakula (IFPRI)Azimio la IFPRI ni kutambua na kutathmini mikakati ya kitaifa na kimataifa na sera za kutosheleza mahitaji ya chakula ya nchi zinazoendelea kwa kiwango kinachoweza kudumishwa, huku wakizingatia zaidi nchi zenye chumi ndogo, watu maskini na usimamizi bora wa mali za asili ambazo ndizo mhimili wa kilimo. 2033 K Street, NW, Washington, DC 20006-1002
(USA) Elimu ya Kimataifa na Ungamo (iEARN)I*EARN ni ungamo la kimataifa la elimu la mawasiliano linalohusisha shule na vikundi vya vijana katika zaidi ya nchi 90 ili kuwezesha wanafunzi kuelewa teknolojia za Mtandao kwa miradi ya pamoja ya masomo kwa kushughulikia masuala ya kitaifa na kimataifa.
I*EARN-USA Shirika la Kujitolea la Kitaifa (NPCA)NPCA ni shirika lisilo la kifaida la watu wa kujitolea, wafanyikazi wa awali na rafiki wa Shirika la Kijitolea miradi na programu za NPCA zinalenga “kuiregesha dunia nyumbani” kupitia shughuli za elimu ya dunia, kujenga amani, huduma na utetezi wa kimataifa. 1900 L Street NW,
Suite 205, Washington DC 20036 (USA) Mradi wa Elimu wa Newsweek (NEP)Azimio la Nep ni kuendeleza kushiriki kwa wanafunzi katika masuala ya siku hizi. Mradi huu unalenga kuboresha ujuzi wa wanafunzi wa uchambuzi wa sera ya umma na kuongeza kushiriki kwao katika mambo na shughuli za kitaifa. NEP hutoa seti za magazeti ya Newsweek kwa shule za upili na madarasa ya vyuo katika lugha ya Kiingereza, Kijamii, Uchumi na ESL. Bei nafuu za wanafunzi pekee huzingatiwa kwa dazani ya makala kama vile ramani, maswali miongozo ya waalimu, vijitabu vya rejea na makala ya kujenga ujuzi. SLP 919 Mountain Lakes, NJ 07046,USA
Chama Cha Umoja wa Mataifa Cha Elimu, Sayansi, na Utamaduni (UNESCO)UNESCO huendeleza umoja na ushirikiano kati ya mataifa kupitia elimu ya sayansi, utamaduni na mawasiliano ili kuheshimu zaidi haki, utawala unaozingatia sheria na haki za binadamu na uhuru halisi unaosisitizwa na Mwafaka wa Umoja wa Mataifa. UNESCO hufanya kazi na waalimu katika viwango vyote na Vyama vingine ili kujumlisha elimu ya kisayansi na kitamaduni na kusaidia wanafunzi kuelewa mazingira yao, chaguzi zao za kijamii na kibinafsi ili kuwezesha kuwepo maendeleo. 7, Place de Fontenoy- Paris 07 SP, France, 75352
(France) Kamati ya Kitaifa ya Kimarekani ya Siku ya Chakula DunianiSiku ya Chakula Duniani ni shughuli ya kila mwaka duniani ambayo nia yake ni kuongeza uelewa, mwaka mzima, wa muda mrefu wa masuala tata ya kuhakikisha kuwepo kwa chakula kwa kila mtu. Kamati ya Kitaifa ya Kimarekani ni muungano wa vyama vya kibinafsi 450 vya kitaifa visivyo vya kifaida vilivyo nchini Marekani. 2175 K Street NW, Washington, DC 20437,
(USA) Benki ya DuniaBenki ya Dunia ndilo shirika kubwa duniani lenye kusaidia katika maendeleo na hutoa
wastani wa dola bilioni 20 zikiwa kama mikopo ya kila mwaka kwa nchi zinazokopeshwa.
Benki hii inatumia raslimali zake za kiuchumi, wafanyaikazi wake wenye ujuzi wa hali ya
juu na elimu yake kubwa kusaidia kila nchi katika usitawi unaoweza kudumishwa
kuhakikisha kuwa kuna ugawaji sawa. Dhima yao kubwa ni kusaidia watu na nchi maskini
zaidi. Katika mandeleo ya mashambani kuna mambo yafuatayo!
1. Kuongeza uzalishaji wa kilimo, kutoa kazi na kuwepo kwa chakula cha
kutosha mashambani. 1818 H Street NW, Washington DC 20433
(USA) WashirikiGlobal Nomads Group
Arab Nutrition Society
Asia-Pacific Network For Food and Nutrition
Secretariat of the Pacific Community
Federación Latinoamericana de Asociaciones Académicos de Nutrición y Dietética
Colegio de Profesores de Chile
Fundación de Vida Rural de la Pontificia, Universidad Católica de Chile
International Institute of Tropical Agriculture
Kenya Coalition for Action in Nutrition
Southern Africa Teachers' Organisation
Societŕ Italiana di Nutrizione Umana
European Food Information Council
World Association of Girl Guides and Girl Scouts
SEE HEALTH (South Eastern Europe Health Promotion Network)
|
Njaa na Ukosefu wa Lishe Bora DunianiUtangulizi wa MwalimuSiku ya Chakula DunianiShukraniKudhaminiWasiliana nasiPata faili la mtindo wa PDF |