Lengo 3: Kujua ni nani mwenye njaa ulimwenguni
Vifaa
Picha:
Ramani ya Njaa Duniani
Dhana :
- Njaa ni kutopata kiasi cha kutosha cha vyakula mwafaka kukidhi
mahitaji yetu
- Nchi zote na maeneo yote yana baadhi ya watu wenye njaa
Yaliyomo
- Njaa ni kutokuwa na chakula cha kutosha na kutokuwa na vyakula tofauti tofauti kukidhi mahitaji yetu ya urutubishi. Njaa ni tatizo duniani kote. Kila nchi na kila eneo lina baadhi ya watu ambao hawapati kiasi cha kutosha cha kula. Ingawa njaa ipo katika kila nchi, baadhi ya nchi na maeneo yana tatizo kubwa zaidi la kuwalisha watu wao.
- Katika mwaka wa 2001, watu milioni 800 wana njaa na hawapi kamwe kiasi cha kutosha cha kula mwaka mzima. Lengo la milenia (kikwi) mpya ni kuhakikisha kuwa kila mtu ana chakula cha kutosha na anakula aina za vyakula zenye kuhitajika (zenye kufaa)
- Njaa ipo kwa sababu nyingi (zimeonyeshwa katika Somo 2) na itachukua kazi kubwa kusuluhisha matatizo ya njaa. Watu wengi wanashirikiana kote duniani na kutafuta uvumbuzi wa tatizo la njaa.
- Watu wote, wakiwemo watoto, wanaweza kuwa sehemu ya juhudi hii kwa kujifunza mengi wawezavyo kuhusu njaa na namna ya kuizuia.
Matendo
- Onyesha Ramani ya Njaa Duniani, yenye kuonyesha maeneo ya njaa kubwa na matatizo ya utapiamlo. Eleza jinsi ramani inaonyesha maeneo ambapo watu wengi hawapati vyakula vyote wanavyohitaji. Bainisha sehemu zenye idadi kubwa zaidi ya watu wenye njaa. Fafanua kuwa nchi zote zina kiasi cha watu wenye njaa.
- Jadili kwamba watu katika kila eneo ambalo kwa kiasi kikubwa huenda wakawa na njaa ni watu wasio na ajira au wasio na elimu, maskini, watu wasio na ardhi ya kupanda vyakula na wale wasiobahatika katika jamii. Watu wengine wawezao kuwa na njaa ni wale wenye mahitaji maalum ya lishe kama vile watoto (wanaohitaji kukua) na akina mama wajawazito na wenye kunyonyesha. Vita, rabsha za kijamii, mabadiliko ya mazingira na dharura nyinginezo kama vile mafuriko na radi aghalabu husababisha njaa ya kipindi kifupi na vilevile kipindi kirefu katika eneo. Tambua eneo/sehemu ya dunia na kujadili tatizo lake la njaa.
- Waulize watoto kuufikiria ulimwengu ambapo watu wote wana chakula cha kutosha cha kula. Waambie wawe ramani ya dunia akilini na kuijadili darasani. Jadili ramani yako akilini na watu wasio na njaa. Palipo na rasilimali waambie wanafunzi kuchora picha ya "Jicho la wazo" ya dunia au mahali ambapo chakula ni kingi na hakuna mtu aliye na njaa na kuipachika picha hii katika majengo ya shule na vilevile katika majengo ya umma katika jamii.
- Jadili jinsi watu wanaweza kukumbwa na njaa kwa sababu nyingi, jinsi inavyochukua juhudi kubwa kulitatua tatizo hili na jinsi watu wengi wanajitahidi kijifunza ni kwa nini watu wana njaa na kutafuta njia za kuhakikisha kuwa kuna chakula kizuri, katika mwaka mzima na kwa kila mtu.
- Jadili jinsi watu ulimwenguni wanaweza kushirikiana ili kila mtu aweze kupata chakula cha kutosha na mwafaka (Kinavyofaa) kuliwa.
Muhtasari
Somo 1 lilitoa vifaa vya kujibu maswali Njaa ni Nini na Wenye Njaa ni Nani? Baada ya
kukamilisha Somo 1 watoto wanahitaji kuweza kueleza kuwa:
- Sote tunahitaji chakula.
- Chakula hutupa nguvu na virutubishi tunavyohitaji ili kukua na kustawi;
kutembea, kuchapa kazi, kucheza, kuwaza na kujifunza; na kudumisha maisha
na afya.
- Chakula kichache sana au kingi sana huleta matatizo ya afya.
- Njaa ni kutopata kiasi cha kutosha cha vyakula vinavyofaa ili kukidhi mahitaji
yetu.
- Maeneo yote yana sehemu ya watu walio na njaa.
- Baadhi ya watu wana mahitaji virutubishi maalum ya lishe, wakiwemo watoto,
akina mama wajawazito na wanaonyonyesha, watu wanaofanya kazi kwa bidii
na walio wagonjwa.
Waeleze wanafunzi kwamba katika somo letu linalofuata tutajifunza kujifunza chakula
kinapotoka na baadhi ya sababu za kwa nini watu wana njaa katika dunia yetu.
Kwa kujiunga na Foramu ya KAKN, bonyeza HAPA.
