KIWANGO CHA MSINGI
Jumla ya muda wa somo: dakika 45
Lengo 1: Kuelewa kwa nini tunahitaji chakula
Dhana:
- Sote tunahitaji chakula
- Chakula hutupa nguvu na virutubishi tunavyohitaji ili kuifanya miili yetu kuendelea kufanya kazi, kukua na kustawi, kutembea, kucheza, kufikiri na kusoma
- Chakula kidogo au kingi mno siyo kizuri kwa afya
Lengo 2: Kujua kuwa tunahitaji aina nyingi tofauti ya vyakula
Dhana:
- Watu wanahitaji aina nyingi tofauti ya vyakula ili kuwa na afya na kukua
Lengo 3: Kujua ni nani mwenye njaa ulimwenguni
Dhana:
- Njaa ni kutopata kiasi cha kutosha cha vyakula mwafaka kukidhi mahitaji yetu
- Nchi zote na maeneo yote yana baadhi ya watu wenye njaa
Jumla ya muda wa somo: dakika 45
Lengo 1: Kuelewa mfumo wa chakula unaowalisha watu
Dhana:
- Mfumo unaotupa chakula unahusisha hatua nyingi
Lengo 2: Kuelewa maana ya kuwa na uhakika wa chakula
Dhana:
-
Kuwa na uthabiti wa chakula ina maana kwamba ni lazima kila wakati tuweze kupata chakula tunachohitaji kwa maisha biabia na yenye afya
- Nguzo tatu za uthabiti wa chakula ni: kupatikana, kufikika na utumiaji wa chakula
Jumla ya muda wa somo: dakika 45
Lengo 1:Kujua kuwa sote tunaweza na lazima tufanye jambo fulani ili kupambana na njaa
Dhana:
- Kili mtu anaweza kuwa shujaa kwa kupambana na njaa
Lengo 2:
Kutambua jinsi ambavyo tunaweza kupambana na njaa katika jamii zetu
Dhana:
- Tunaweza kutenda jambo fulani ili kusaidia kumaliza njaa